Yapo madai mbalimbali kwamba maiti zinazokosa ndugu na kulazimika kuzikwa na manispaa, huwa hazipewi heshima inayostahili, ikiwa ni pamoja na maiti zaidi ya moja kuzikwa kwenye kaburi moja, baadhi kukatwa viungo na nyingine kufukiwa kama inavyofukiwa mizoga ya wanyama.
Kufuatia madai hayo ambayo yapo kwenye jamii kwa muda mrefu, gazeti hili liliamua kuanza uchunguzi wa kina kubaini kama yana ukweli wowote, na kama ni kweli, ni nani hasa anayehusika na unyama huo?
MAKABURI YA KINONDONI
Uchunguzi unaanzia kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo gazeti hili linakutana ana kwa ana na msimamizi wa makaburi hayo, ambaye pia hushiriki kwenye zoezi la kuzika maiti za namna hiyo, Omary Nassibu.
Mbali na mambo mengine, msimamizi huyo anamueleza mwandishi wa ripoti hii kusikitishwa na madai hayo ambayo naye anakiri kuwahi kuyasikia lakini anasita kutoa ufafanuzi wa kina kwa sababu yeye si msemaji wa serikali.
“Nakushauri uende ukaonane na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni au Mkurugenzi wa Jiji, akikupa ruhusa ya maandishi, ndipo nitakapokuwa tayari kukufafanulia kwa kina kuhusu madai hayo na Watanzania wote wataujua ukweli,” anasema Nassibu.
Mwandishi wetu anafuata maelekezo ya Nassibu ya kuandika barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni na Mkurugenzi wa Jiji na siku kadhaa baadaye, anaenda kuonana na mkurugenzi wa manispaa ambaye naye, anamuelekeza kwenda kukutana na Afisa Afya wa Manispaa ya Kinondoni, Mathias Nemes Kapizo.
Kapizo kimsingi ndiyo msimamizi wa shughuli zote za kiafya wilayani humo na pia ndiye anayeratibu na kusimamia maiti zinazozikwa na manispaa.
OFISINI KWA AFISA AFYA WA MANISPAA
Baada ya kufika ofisini kwa Kapizo, alitoa ushirikiano mzuri kwa mwandishi wetu na yafuatayo ni maelezo aliyoyatoa kulingana na maswali aliyokuwa anaulizwa:
Swali: Ni maiti za namna gani zinazozikwa na manispaa?
Kapizo: Hapa huwa tunashughulika na maiti zisizokuwa na ndugu, maiti za ajali ambazo zimeharibika kiasi cha kutotambulika na zile zinazotokana na magonjwa hatari kama Ebola, Kipindupindu na magonjwa mengine kama hayo.
Nyingine ni zile zilizotelekezwa na ndugu zao hospitalini. Unakuta mgonjwa ametoka kwa mfano Kigoma, kabla ya kufikishwa Dar es Salaam, ameshapitia kuanzia kwa waganga wa kienyeji na kwenye hospitali mbalimbali ambako kote alikuwa akitoa fedha.
Mtu wa namna hii, unakuta ndugu zake wameshatumia fedha nyingi sana mpaka akija kufika kwenye hospitali za hapa, ndugu wanakuwa wameishiwa. Kwenye hospitali zetu za serikali si unajua mgonjwa akilazwa anatakiwa kulipia kila siku?
Na kama ikitokea amefariki, ndugu hawawezi kupewa maiti mpaka wawe wamelipa deni, sasa wengi wakifikia hatua hii, huwa wanakimbia na kutelekeza maiti wodini kwa kuwa wanakuwa hawana fedha za kulipa deni wala za kusafirisha. Maiti za namna hii huwa tunazizika pia.
KUHUSU WANAOKUFA KWA KIPINDUPINDU, EBOLA
Swali: Ni tahadhari gani huwa mnazichukua mnapozika maiti za watu waliokufa kutokana na magonjwa hatari kama Ebola na Kipindupindu?
Kapizo: Hakuna kazi ngumu kama hiyo kwa sababu kitaalam, maiti ya aina hiyo haitakiwi hata kuingizwa mochwari, madaktari wakishathibitisha amekufa ni moja kwa moja anatakiwa kwenda kuzikwa.
Tahadhari ni kuvaa mavazi maalum ya kuzuia uambukizo na kuhakikisha watu wasiohusika hawasogei kabisa kwenye eneo la mazishi. Changamoto kubwa katika hili huwa ni vifaa vya kutendea kazi, yakiwemo mavazi maalum na madawa ya kujikinga.
Swali: Kwa wastani mnazika maiti ngapi kwa mwezi?
Kapizo: Siwezi kusema ni maiti ngapi kwa sababu siku zinatofautiana, kukiwa na ajali nyingi au magonjwa ya milipuko huwa tunazika wengi lakini siku ambazo hayo hayapo, kwa wastani huwa ni maiti tano hadi sita kwa mwezi.
KUHUSU UDHALILISHAJI WA MAITI
Swali: Yapo madai kwamba maiti zisizo na ndugu huzikwa zaidi ya moja kwenye kaburi moja na wakati mwingine, nyingine hukatwa miguu au mikono ili zote ziingie kwenye kaburi moja. Unalizungumziaje hili?
Kapizo: Hakuna kitu kama hicho hata kidogo. Hao wanaozusha maneno hayo, wanapaswa kupimwa akili zao. Ndugu mwandishi, mfano mwepesi tu, huko barabarani si kila siku huwa unaona mizoga ya wanyama kama mbwa na wengine? Je, umewahi kuona mzoga wa mbwa unakatwa miguu kisha ndiyo unafukiwa?
Kufuatia madai hayo ambayo yapo kwenye jamii kwa muda mrefu, gazeti hili liliamua kuanza uchunguzi wa kina kubaini kama yana ukweli wowote, na kama ni kweli, ni nani hasa anayehusika na unyama huo?
MAKABURI YA KINONDONI
Uchunguzi unaanzia kwenye Makaburi ya Kinondoni jijini Dar es Salaam ambapo gazeti hili linakutana ana kwa ana na msimamizi wa makaburi hayo, ambaye pia hushiriki kwenye zoezi la kuzika maiti za namna hiyo, Omary Nassibu.
Mbali na mambo mengine, msimamizi huyo anamueleza mwandishi wa ripoti hii kusikitishwa na madai hayo ambayo naye anakiri kuwahi kuyasikia lakini anasita kutoa ufafanuzi wa kina kwa sababu yeye si msemaji wa serikali.
“Nakushauri uende ukaonane na Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni au Mkurugenzi wa Jiji, akikupa ruhusa ya maandishi, ndipo nitakapokuwa tayari kukufafanulia kwa kina kuhusu madai hayo na Watanzania wote wataujua ukweli,” anasema Nassibu.
Mwandishi wetu anafuata maelekezo ya Nassibu ya kuandika barua kwenda kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni na Mkurugenzi wa Jiji na siku kadhaa baadaye, anaenda kuonana na mkurugenzi wa manispaa ambaye naye, anamuelekeza kwenda kukutana na Afisa Afya wa Manispaa ya Kinondoni, Mathias Nemes Kapizo.
Kapizo kimsingi ndiyo msimamizi wa shughuli zote za kiafya wilayani humo na pia ndiye anayeratibu na kusimamia maiti zinazozikwa na manispaa.
OFISINI KWA AFISA AFYA WA MANISPAA
Baada ya kufika ofisini kwa Kapizo, alitoa ushirikiano mzuri kwa mwandishi wetu na yafuatayo ni maelezo aliyoyatoa kulingana na maswali aliyokuwa anaulizwa:
Swali: Ni maiti za namna gani zinazozikwa na manispaa?
Kapizo: Hapa huwa tunashughulika na maiti zisizokuwa na ndugu, maiti za ajali ambazo zimeharibika kiasi cha kutotambulika na zile zinazotokana na magonjwa hatari kama Ebola, Kipindupindu na magonjwa mengine kama hayo.
Nyingine ni zile zilizotelekezwa na ndugu zao hospitalini. Unakuta mgonjwa ametoka kwa mfano Kigoma, kabla ya kufikishwa Dar es Salaam, ameshapitia kuanzia kwa waganga wa kienyeji na kwenye hospitali mbalimbali ambako kote alikuwa akitoa fedha.
Mtu wa namna hii, unakuta ndugu zake wameshatumia fedha nyingi sana mpaka akija kufika kwenye hospitali za hapa, ndugu wanakuwa wameishiwa. Kwenye hospitali zetu za serikali si unajua mgonjwa akilazwa anatakiwa kulipia kila siku?
Na kama ikitokea amefariki, ndugu hawawezi kupewa maiti mpaka wawe wamelipa deni, sasa wengi wakifikia hatua hii, huwa wanakimbia na kutelekeza maiti wodini kwa kuwa wanakuwa hawana fedha za kulipa deni wala za kusafirisha. Maiti za namna hii huwa tunazizika pia.
KUHUSU WANAOKUFA KWA KIPINDUPINDU, EBOLA
Swali: Ni tahadhari gani huwa mnazichukua mnapozika maiti za watu waliokufa kutokana na magonjwa hatari kama Ebola na Kipindupindu?
Kapizo: Hakuna kazi ngumu kama hiyo kwa sababu kitaalam, maiti ya aina hiyo haitakiwi hata kuingizwa mochwari, madaktari wakishathibitisha amekufa ni moja kwa moja anatakiwa kwenda kuzikwa.
Tahadhari ni kuvaa mavazi maalum ya kuzuia uambukizo na kuhakikisha watu wasiohusika hawasogei kabisa kwenye eneo la mazishi. Changamoto kubwa katika hili huwa ni vifaa vya kutendea kazi, yakiwemo mavazi maalum na madawa ya kujikinga.
Swali: Kwa wastani mnazika maiti ngapi kwa mwezi?
Kapizo: Siwezi kusema ni maiti ngapi kwa sababu siku zinatofautiana, kukiwa na ajali nyingi au magonjwa ya milipuko huwa tunazika wengi lakini siku ambazo hayo hayapo, kwa wastani huwa ni maiti tano hadi sita kwa mwezi.
KUHUSU UDHALILISHAJI WA MAITI
Swali: Yapo madai kwamba maiti zisizo na ndugu huzikwa zaidi ya moja kwenye kaburi moja na wakati mwingine, nyingine hukatwa miguu au mikono ili zote ziingie kwenye kaburi moja. Unalizungumziaje hili?
Kapizo: Hakuna kitu kama hicho hata kidogo. Hao wanaozusha maneno hayo, wanapaswa kupimwa akili zao. Ndugu mwandishi, mfano mwepesi tu, huko barabarani si kila siku huwa unaona mizoga ya wanyama kama mbwa na wengine? Je, umewahi kuona mzoga wa mbwa unakatwa miguu kisha ndiyo unafukiwa?
COOPERATIVES
A cooperative is an organised group of like-minded producers who combine to form a farmers’ group or partnership. Members share responsibilities and any profit or loss. They speak with a single voice and can purchase feed, equipment, chicks, building material and other supplies more cheaply. Eventually storage facilities can be established and a supply shop set up. The group can also have a strategic plan to reduce competition between individuals, set prices for poultry products and generally work to help one another to establish an industry on a firm footing. Trainers should provide as much assistance as possible to the farmers in establishing a working group that will spearhead the formation of a cooperative. The cooperative may eventually expand into other areas of commerce where the farmers can trade other farm produce in addition to poultry.COMMUNITY OWNERSHIP
This is similar to, but less rigid than a cooperative and is run by a committee representing a district or village community. For example, the committee may be responsible for raising point - of - lay pullets. These they sell at 17 - 18 weeks to individual egg producers and the profits are distributed amongst the community. The committee might purchase and run an incubator, and sell the chicks for meat or egg production at different ages. Or the committee may manage a small broiler or egg farm along commercial lines. In both cases there is opportunity to buy large numbers of chicks and bags of feed. This is usually attractive to the supplier and cheaper for the community. The concept of community farming is to empower people, mainly women, who have no opportunity as individual poultry keepers, to improve their circumstances and to alleviate poverty. Once formed, It can be extended to bio-security programs, vaccination programs against diseases, purchase of medical and other supplies, marketing of meat birds and eggs, dissemination of information, training programs and exchanging information, and greater opportunity to obtain micro-credit. This is critical to allow expansion of the family enterprise. There is a key role here for the poultry trainer who can assist in orchestrating the group by providing advice and guidance.BE THE FIRST TO COMMENT


