DAR ES SALAAM: Wakati nafasi za wakurugenzi sita, mameneja watano na mhandisi mmoja wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) zilizoachwa wazi baada ya wahusika kusimamishwa zikiwa tayari zimejazwa, Uwazi limeuchimba kwa kina mradi uliowaponza vigogo hao waliosimamishwa hivi karibuni.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, mwandishi wetu alifunga safari mpaka Dege, uliko mradi wa Ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni (Dege Eco Village) – (pichani) ambao unatajwa kuwa ndiyo uliosababisha kutumbuliwa kwa vigogo hao na kuzungumza na wakandarasi na wafanyakazi waliokuwa wakishiriki kwenye mradi huo.
WALIANZA HIVI
“Huu mradi kwa kweli ulikuwa na figisufigisu nyingi sana. Mimi binafsi nilikuwa nafanya kazi kama kibarua na kuna mambo mengi tu nilikuwa naona hayaendi sawa,” kilisema chanzo kimoja kilichoomba hifadhi ya jina lake.
Chanzo hicho kiliendelea kutiririka kwamba, kabla ya kuanza kwa mradi huo, eneo halikuwa na shughuli yoyote ya msingi lakini mradi ulipoanza, vigogo wengi serikalini, walianza kununua viwanja vikubwa kwenye maeneo ya kuzunguka mradi na kuporomosha majumba ya kifahari.
“Si unaona majumba ya watu binafsi yalivyoporomoshwa kwa wingi upande wa pili wa mradi? Hawa wote hakuna mkazi wa Dege hata mmoja, ni watu wa serikalini. Mradi wenyewe una magorofa kama 40 hivi,” kiliendelea kutiririka chanzo chetu.
MAFUNDI WALIUTABIRIA
Fundi mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la James, yeye alisema walishajua kwamba mradi huo hauwezi kukamilika kutokana na mambo mbalimbali yaliyoashiria hivyo (hakuyasema).
“Unajua kabla mradi haujasimamishwa, tulikuwa tunafanya kazi sehemu mbilimbili, yaani kwenye mradi na kwenye nyumba za baadhi ya vigogo wa serikalini. Kwa hiyo tulihisi kuna mambo hayaendi sawasawa sana.
“Mi naona hata serikali yenyewe ilichelewa kushtuka mapema. Lakini kwa vile wamesimamishwa, uchunguzi ufanyike kuona nani alikosa, naamini wapo waliosimamishwa hawahusiki lakini kuna wanaohusika, wapo kazini,” alisema fundi huyo.
Baada ya kusikia maelezo hayo, Uwazi lilifanya jitihada za kuwapata vigogo waliotumbuliwa. Hata hivyo, kazi ya kuwapata vigogo hao ana kwa ana haikuwa nyepesi.
Uwazi lilifanikiwa kupanga ‘appointment’ ya kukutana na Yacob Kidula, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi ambapo licha ya makubaliano ya kukutana, simu ya kigogo huyo haikuwa ikipatikana hewani na hata ilipopatikana, haikuwa ikipokelewa
Mwandishi wetu alifanya jitihada za kumtumia ujumbe wa maandishi kigogo huyo akimsisitiza kuhusu kukutana naye au kuzungumza chochote kuhusu kusimamishwa kwake lakini hakujibu mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni.
KUTOTAKA KUZUNGUMZA
Kuna taarifa kuwa, vigogo hao hawako tayari kuzungumza lolote kwa vile, suala lao linachunguzwa na vyombo husika ili kubaini ukweli wa madai yao na endapo wataonekana hawana hatia, watarudishwa kazini.
Hivi karibuni, bodi ya wadhamini ya NSSF inayoongozwa na Profesa Samuel Wangwe, iliagiza kusimamishwa kazi kwa wakurugenzi sita, mameneja watano na mhandisi mmoja wa shirika hilo ili kupisha uchunguzi baada ya kubainika kuwepo kwa vitendo vya ubadhirifu, matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata kanuni, sheria na taratibu katika uwekezaji, usimamizi wa miradi, manunuzi ya ardhi na ajira.
Wakurugenzi sita waliosimamishwa kazi na nafasi zao kwenye mabano ni Kidula (Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi), Ludovick Mrosso (Mkurugenzi wa Fedha), Chiku Matessa (Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala) na Sadi Shemilwa (Mkurugenzi wa Udhibiti Hadhara na Majanga).
Wengine ni Pauline Mtunda (Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Mahesabu ya Ndani) na Crescentius Magori (Mkurugenzi wa Uendeshaji) sambambana mameneja wengine watano na mhandisi mmoja.
Kabla ya kutumbuliwa vigogo hao, mradi huo ulisimamishwa na serikali Aprili, mwaka huu baada ya kubainika kuwepo kwa upotevu wa zaidi ya shilingi bilioni 179.
Mradi huo ulikuwa ukisimamiwa na Kampuni ya Hifadhi Builders LTD iliyokuwa chini ya NSSF kwa ushirikiano wa Azimio Housing Estate Limited, mkandarasi akiwa ni M/s Mutluhan Construction Industry Company Limited kutoka Uturuki.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, mwandishi wetu alifunga safari mpaka Dege, uliko mradi wa Ujenzi wa Mji Mpya wa Kigamboni (Dege Eco Village) – (pichani) ambao unatajwa kuwa ndiyo uliosababisha kutumbuliwa kwa vigogo hao na kuzungumza na wakandarasi na wafanyakazi waliokuwa wakishiriki kwenye mradi huo.
WALIANZA HIVI
“Huu mradi kwa kweli ulikuwa na figisufigisu nyingi sana. Mimi binafsi nilikuwa nafanya kazi kama kibarua na kuna mambo mengi tu nilikuwa naona hayaendi sawa,” kilisema chanzo kimoja kilichoomba hifadhi ya jina lake.
Chanzo hicho kiliendelea kutiririka kwamba, kabla ya kuanza kwa mradi huo, eneo halikuwa na shughuli yoyote ya msingi lakini mradi ulipoanza, vigogo wengi serikalini, walianza kununua viwanja vikubwa kwenye maeneo ya kuzunguka mradi na kuporomosha majumba ya kifahari.
“Si unaona majumba ya watu binafsi yalivyoporomoshwa kwa wingi upande wa pili wa mradi? Hawa wote hakuna mkazi wa Dege hata mmoja, ni watu wa serikalini. Mradi wenyewe una magorofa kama 40 hivi,” kiliendelea kutiririka chanzo chetu.
MAFUNDI WALIUTABIRIA
Fundi mwingine aliyejitambulisha kwa jina moja la James, yeye alisema walishajua kwamba mradi huo hauwezi kukamilika kutokana na mambo mbalimbali yaliyoashiria hivyo (hakuyasema).
“Unajua kabla mradi haujasimamishwa, tulikuwa tunafanya kazi sehemu mbilimbili, yaani kwenye mradi na kwenye nyumba za baadhi ya vigogo wa serikalini. Kwa hiyo tulihisi kuna mambo hayaendi sawasawa sana.
“Mi naona hata serikali yenyewe ilichelewa kushtuka mapema. Lakini kwa vile wamesimamishwa, uchunguzi ufanyike kuona nani alikosa, naamini wapo waliosimamishwa hawahusiki lakini kuna wanaohusika, wapo kazini,” alisema fundi huyo.
Baada ya kusikia maelezo hayo, Uwazi lilifanya jitihada za kuwapata vigogo waliotumbuliwa. Hata hivyo, kazi ya kuwapata vigogo hao ana kwa ana haikuwa nyepesi.
Uwazi lilifanikiwa kupanga ‘appointment’ ya kukutana na Yacob Kidula, aliyekuwa Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi ambapo licha ya makubaliano ya kukutana, simu ya kigogo huyo haikuwa ikipatikana hewani na hata ilipopatikana, haikuwa ikipokelewa
Mwandishi wetu alifanya jitihada za kumtumia ujumbe wa maandishi kigogo huyo akimsisitiza kuhusu kukutana naye au kuzungumza chochote kuhusu kusimamishwa kwake lakini hakujibu mpaka gazeti hili linakwenda mitamboni.
KUTOTAKA KUZUNGUMZA
Kuna taarifa kuwa, vigogo hao hawako tayari kuzungumza lolote kwa vile, suala lao linachunguzwa na vyombo husika ili kubaini ukweli wa madai yao na endapo wataonekana hawana hatia, watarudishwa kazini.
Hivi karibuni, bodi ya wadhamini ya NSSF inayoongozwa na Profesa Samuel Wangwe, iliagiza kusimamishwa kazi kwa wakurugenzi sita, mameneja watano na mhandisi mmoja wa shirika hilo ili kupisha uchunguzi baada ya kubainika kuwepo kwa vitendo vya ubadhirifu, matumizi mabaya ya ofisi na kutofuata kanuni, sheria na taratibu katika uwekezaji, usimamizi wa miradi, manunuzi ya ardhi na ajira.
Wakurugenzi sita waliosimamishwa kazi na nafasi zao kwenye mabano ni Kidula (Mkurugenzi wa Mipango, Uwekezaji na Miradi), Ludovick Mrosso (Mkurugenzi wa Fedha), Chiku Matessa (Mkurugenzi wa Rasilimali Watu na Utawala) na Sadi Shemilwa (Mkurugenzi wa Udhibiti Hadhara na Majanga).
Wengine ni Pauline Mtunda (Mkurugenzi wa Ukaguzi wa Mahesabu ya Ndani) na Crescentius Magori (Mkurugenzi wa Uendeshaji) sambambana mameneja wengine watano na mhandisi mmoja.
Kabla ya kutumbuliwa vigogo hao, mradi huo ulisimamishwa na serikali Aprili, mwaka huu baada ya kubainika kuwepo kwa upotevu wa zaidi ya shilingi bilioni 179.
Mradi huo ulikuwa ukisimamiwa na Kampuni ya Hifadhi Builders LTD iliyokuwa chini ya NSSF kwa ushirikiano wa Azimio Housing Estate Limited, mkandarasi akiwa ni M/s Mutluhan Construction Industry Company Limited kutoka Uturuki.
COOPERATIVES
A cooperative is an organised group of like-minded producers who combine to form a farmers’ group or partnership. Members share responsibilities and any profit or loss. They speak with a single voice and can purchase feed, equipment, chicks, building material and other supplies more cheaply. Eventually storage facilities can be established and a supply shop set up. The group can also have a strategic plan to reduce competition between individuals, set prices for poultry products and generally work to help one another to establish an industry on a firm footing. Trainers should provide as much assistance as possible to the farmers in establishing a working group that will spearhead the formation of a cooperative. The cooperative may eventually expand into other areas of commerce where the farmers can trade other farm produce in addition to poultry.COMMUNITY OWNERSHIP
This is similar to, but less rigid than a cooperative and is run by a committee representing a district or village community. For example, the committee may be responsible for raising point - of - lay pullets. These they sell at 17 - 18 weeks to individual egg producers and the profits are distributed amongst the community. The committee might purchase and run an incubator, and sell the chicks for meat or egg production at different ages. Or the committee may manage a small broiler or egg farm along commercial lines. In both cases there is opportunity to buy large numbers of chicks and bags of feed. This is usually attractive to the supplier and cheaper for the community. The concept of community farming is to empower people, mainly women, who have no opportunity as individual poultry keepers, to improve their circumstances and to alleviate poverty. Once formed, It can be extended to bio-security programs, vaccination programs against diseases, purchase of medical and other supplies, marketing of meat birds and eggs, dissemination of information, training programs and exchanging information, and greater opportunity to obtain micro-credit. This is critical to allow expansion of the family enterprise. There is a key role here for the poultry trainer who can assist in orchestrating the group by providing advice and guidance.BE THE FIRST TO COMMENT

